Visitors


hit counter

Breaking News

728-banner


web counter

OnAir

Friday 29 November 2013

HII KALI KWA DIAMOND PLATNUMZ!!! AAMUA KUJIITA 'DOMO' INSTAGRAM...CHEKI HAPA


Diamond Platnumz aka Prezident wa WCB ametoa kali na mpya kwa kuamua kujiita 'DoMo' kupitia ukurasa wake wa Instagram kama unavyo ona hapo chini. Yawezekana amefikia hatua hiyo baada ya watu wengi kumkashifu mara nyingi sababu ya mdomo wake. 


Kwangu mimi sioni tatizo maana ndivyo alivyo umbwa na je alikuwa anauliza wakuandika hivyo kweli? Au ndo kutupa cha kuongela? All in all he rocks big time being one of the most successful artists in East Africa pamoja na 'DoMo'
Read more ...

BABA KANUMBA ATOA MASHARTI MAGUMU KWA WALE WOTE WANAOTAKA UZAO WAJITOKEZA, WATIMKA

Baba wa marehemu Steven Kanumba, Charles Kusekwa.


BABA wa marehemu Steven Kanumba, Charles Kusekwa amefunguka kuwa baada ya kutangaza kuwa wanawake wanaotaka uzao wake wajitokeze azae nao, wamejitokeza kumi lakini akawapa masharti, yakawashinda.
Akizungumza na mwandishi wetu, baba Kanumba aliweka bayana kuwa warembo hao waliojitokeza aliwapa sharti la kwenda kupima Ukimwi lakini ajabu wote waliingia mitini.
“Wamejitokeza vizuri lakini nashangaa wote wamekuwa wazito katika suala la kupima Ukimwi wameingia mitini, kama wapo wengine watakaolimudu sharti hilo, nawakaribisha,” alisema baba Kanumba

Read more ...

Picha sita za muonekano wa jengo jipya la uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) baada ya ujenzi Utakapokamilika



Hapa ni mahali ambapo abiria watakuwa wakisubiri kabla ya kwenda kupanda ndege (Departure Lounge)

Muonekano wa ndani ya jengo

 Jinsi patakavyoonekana kutokea angani





Upande wa maegesho ya ndege
Ujenzi wa jengo hilo umepangwa kufanyika kwa awamu mbili. Kukamilika kwa awamu ya kwanza kutawezesha uwanja huo kufikia uwezo wa abiria mil 3.5 kwa mwaka tofauti na jengo la sasa ambalo uwezo wake ni abiria mil 1.5 kwa mwaka. Awamu ya pili itaongeza uwezo huo hadi kufikia abiria mil 6 kwa mwaka. Baada ya kukamilika jengo hilo, jengo lililopo sasa (Terminal II) litatumika kwa shughuli za abiria wanaosafiri ndani ya Tanzania tu.

Read more ...

"Yaliyotokea kwenye Msiba wa Sharo Milionea sitakati yajirudie kwangu siku Nikifa"....Kitale


Muigizaji na mwimbaji nchini Kitale yuko Tanga alipoenda kuhudhuria Dua ya kumuombea marehemu Sharo Milionea ikiwa ni mwaka mmoja tangu afariki dunia kwa ajali mbaya ya gari.

Kitale ambaye ndiye msanii pekee aliyefika Tanga siku ya juzi amesema kuwa amejifunza mambo mengi katika msiba wa rafiki yake Sharo Milionea, ikiwa ni pamoja na misiba ya wasanii wengine waliotangulia mbele ya haki, Kanumba na Sajuki.

Akiongea kwa njia ya simu na Edson Mkisi katika kipindi cha Hatua Tatu cha 100.5 Times Fm, Kitale amesema kutokana na funzo alilopata ameampa ujumbe mama yake ili kwamba pindi atakapotangulia mbele ya haki mambo hayo yasijirudie kwake.

“Nimejifunza vitu vingi na nimejua marafiki walio wema na marafiki wasio wema. Ina maana kwamba kuna marafiki wanafiki na marafiki wasio wanafiki. Amesema Kitale.

“Kuna vitu vingi nimejifunza baada ya kuondoka marehemu Steven Kanumba, nimejifunza baada ya kifo cha Sharo Milionea, na nimejifunza baada ya kifo cha Sajuki. Nimejifunza vitu vingi sana sana sana.” Amesisitiza.

 “Ina maana hata mimi kama ntatangulia kuna mambo ambayo nimeshamweleza mama yangu na nimeshaieleza familia yangu, nafikiri hakitakuja kutokea kama kilichotokea kwa wenzangu. Nimejifunza vitu vingi hasa ukiwa msanii...” Kitale ameiambia Hatua Tatu.

Hata hivyo Kitale alikataa kueleza ujumbe huo na kudai kuwa ni siri kati yake na familia yake kwa kuwa hafahamu nani atatangulia kati yake na wazazi wake.
Kitale amewashauri wasanii kumkumbuka Mungu wakati wanapoendelea na shughuli zao na ndio sababu watu wengi wanaamini kuwa asilimia kubwa ya wasanii ni ‘Freemason’, na kwamba hiyo inatokana na kitendo cha wasanii hao kumsahamu Mungu wao.

(November 27,2012) ndio siku ambayo marehemu Sharo Milionea alizikwa huko Tanga.
Read more ...

WATUMIA NYETI YA MWANAUME KAMA KEKI YA BIRTHDAY.......CHEKI HAPA!!


Katika hali inayozidi kuonesha kuporomoka kwa maadili na heshima miongoni mwa wanawake,
wasanii fulani nchini Nigeria wamefanya kali ya mwaka pale walipotengeza keki ya Birthday ya rafiki yao ambayo ilipambwa na taswira ya NYETI za kiume ambapo rafiki huyo alikuwa akiilamba kila wakati kama anavyoonekana pichani hapo juu
Read more ...

KWANINI BAADHI YA WATU WANACHUKIA MAFANIKIO YA DIAMOND? ...TATIZO NI ‘BEI YA MKAA’....SOMA ZAIDI HAPA


Wakati mwingine inahitaji roho ya paka kuendelea na nguvu kufanya kile unachofanya wakati watu wanaendelea kukudhihaki.
Zaidi ya muziki, kuna kitu gani kizuri kinachoitangaza Tanzania nje ya nchi kwa sasa? Tusaidiane kuuchambua ukweli huu unaomezeka kwa fundo la mate la kulazimisha kinywani.
 Ni lini mara ya mwisho Tanzania imefanya vizuri kimataifa kwenye soka? Hakuna habari njema zaidi ya kuendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu, iwe kwetu hata nje


Ni lini mara ya mwisho mkimbiaji riadha wa Tanzania ameshinda mbio zozote za kimataifa? Hakuna.
Kimichezo ni kama bado tumeendelea kuwa wasindikizaji tu. Au umesahau jinsi Selemani Kidunda alivyodundwa mwaka 2012 kwenye mashindano ya Olimpiki? Ukitoa mwaka 2005 pale Nancy Sumari alipokuwa Miss World Afrika, ni lini mrembo yeyote wa Tanzania amewahi kuiletea sifa nchi yetu?

Ni nini hasa kinachoweza kuifanya Tanzania kuipeperusha bendera yake kwenye jukwaa la kimataifa kwa sifa nzuri? Au labda kipindi hiki tumegeuka kuwa mabingwa wa biashara ya dawa za kulevya na Watanzania ndio wamekuwa vinara wa kukamatwa kila kukicha nchi za nje.

Angekuwepo Kanumba na zile jitihada alizokuwa akizifanya, labda tungesema Bongo Movies ilikuwa inaelekea kuwa njia nzuri ya kutupa heshima pia. Lakini tangu afariki, hakuna mwingine anayeonesha dalili za kufanya kile alichokuwa anakifanya na filamu zetu zimeendelea kuwa za nyumbani pekee.
Hivyo, ukiangalia kwa mifano hiyo, ni muziki pekee wenye matumaini ya kuliongezea ‘kiki’ jina la nchi yetu kwenye ‘google search’. Lakini kama muziki ndio unaonekana kuwa kitu muhimu kinachoitangaza Tanzania, mbona wale wanaofanya vizuri kwa kutuwakilisha nje tunawabeza?

Mpaka muda huu, ukimtoa AY, hakuna msanii mwingine wa Tanzania anayevuma kimataifa kama alivyo Diamond Platnumz. Amefanikiwa kiasi cha hivi karibuni kumshirikisha staa wa Nigeria Davido kwenye remix ya wimbo wake, Number 1 na video iliyogharimu si chini ya dola 25,000 iko mbioni kutoka. Amekuwa ni msanii mwenye kujituma, kutake risk na kutochoka kujaribu kufanya kile wengi wamekuwa wakikiogopa kufanya. Lakini bado kuna watu wengi hawaoni anachokifanya na wameendelea kumkejeli.
Wanasema hakuna binadamu aliye mkamilifu, lakini pamoja na kwamba unaweza kumnyonga mnyonge, ni vyema kukumbuka kumpa haki yake. Ni asili ya mwanadamu kuumizwa na mafanikio ya mtu mwingine, na ndio kinachotokea kwa Diamond. Ameendelea kufanikiwa kiasi mpaka anaanza kuwakera wengine. Si kosa kuchukia maisha na scandal zake, lakini si kosa pia kusifia kile anachoifanyia Tanzania.
Read more ...

TID KUFANYA COLLABO NA MWANADADA MREMBO NA MWENYE KUVUTIA" AZEB WENDWOSEN" KUTOKA ETHIOPIA


Khalid Mohamed aka TID (Top in Dar) ametangaza kufanya collabo na msanii mrembo wa Ethiopia aitwaye Azeb Wendwosen.“She is called Azeb an Ethiopian Artist who is duin a single with me currently…” TID mnyama ameandika kupitia Instagram na kuweka picha ya msanii huyo mrembo kwelikweli.
Baada ya kumtafuta kwa simu kuzungumiza swala hilo big boss huyo wa Top Band amesema atatoa taarifa kamili juu ya collabo hiyo soon.

Tazama picha zake hapa




Read more ...

TAMBUA MADHARA YA KUTOSHIRIKI TENDO LA NDOA KWA MUDA MREFU...(18+)


Aise, kwa kawaida kama wewe si mgonjwa wa aina yoyote ile, kwa maana ya ugonjwa ku-offset system ya mwili, madhara ya kutofanya tendo la ndoa kwa muda mrefu ni makubwa kuliko unavyofikiria as long as upo ktk active range of age! madhara yapo ya Negative na positive.


Mfumo wa fahamu (central novous system) hutumia zaidi tendo la ndoa ku-radiate energy inayowezesha ubongo pamoja na mifumo mingine ya mwili kufanya kazi zake vizuri bila msongo. Suala hapa si lazima uke na uume kukutana na kuingiliana (penetration) ila tu stimulation(msisimko) inayofikisha mtu
kileleni (orgasms). kwahiyo, nature(asili) inataka mke na mme kufanikisha zoezi hili maana ni jambo muhimu kama ilivyo kutoka jasho mwilini maana sio tu mwili unaondoa uchafu ndani lakini pia inacontrol joto la mwili (cooling effect).


Anayesema amekaa zaidi ya mwaka na hana madhara.., well sikatai wala sikubali maana hatuna ushahidi nalo lakini zipo njia nyingi mbadala kama kutumia sex toys, 
dildo(vibrant artificial penis zitumiazo umeme), usagaji n.k. sasa sijui yeye anatumia ipi sababu vichocheo anavyo mwilini and, it's brain iniciated.


Ukidumu bila tendo la ndoa muda mrefu, baadhi ya madhara madogomadogo nikama haya:
Hasira za mara kwa mara ktk mambo madogo,
kupendelea sana kuangalia picha za uchi,
Kusahausahau,
Kupendelea story za mapenzi,
Kutokwa damu nyingi wakati wa hedhi (Mke),
Kupenda kurukiarukia mambo ya watu wengine (tabia ya kufuatilia mambo yasiyokuhusu),
Kuumwa na kichwa,
Kukakamaa mgongo (wanaume),
Kuingiliwa kirahisi na jini mahaba,
Kupoteza umakini ktk kazi (efficiency),
Siku ukikutana kimwili na mwenye virusi bila kinga utaambukizwa kirahisi mno,
Waweza ku-develop tabia mpya ambayo hukuwahi kuwa nayo ili iwe mbadala kama ulevi…
Read more ...

MAMBO YAMEANZA!! ZITTO KABWE AANZA KUMSHUGHULIKIA MMOJA BAADA YA MWINGINE, AMPANDISHA POLISI HENRY KILEWO


WAKATI Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kikimwandikia Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe barua ya kumtaka ajieleze dhidi ya tuhuma zinazomkabili, yeye ameamua kukimbilia polisi akimshitaki mmoja wa viongozi wenzake.

Habari za kuaminika zimedai kuwa Zitto ambaye hivi karibuni alivuliwa cheo chake cha unaibu katibu mkuu wa CHADEMA, inadaiwa amefungua mashitaka polisi akimtuhumu Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Dar es Salaam, Henry Kileo kwa madai ya kusambaza waraka katika mitandao ya kijamii.
 
Akithibitisha tukio hilo, wakili wa Kileo, Peter Kibatara, alisema kuwa mteja wake amemriwa kufika makao makuu ya Jeshi la Polisi leo Jumatano saa nane mchana na kuonana na mmoja wa maofisa wa juu wa jeshi hilo, aliyetajwa kwa jina moja tu la Mbutta, kufuatia mashitaka yaliyofunguliwa na Zitto dhidi yake.
 
Akizungumza kwa njia ya simu na mwandishi wetu, Kileo alikiri kuitwa polisi, ingawa alidai hajui ni waraka gani anaotuhumiwa kuusambaza unaomchafua Zitto.
 
“Kwa kweli sijui hata mimi ni waraka gani, ingawa hivi karibuni kulikuwa na waraka wa siri uliodaiwa kutoka CHADEMA, na ambao ulijaa tuhuma za usaliti. Lakini huo tuliishaukana siku nyingi. Labda kuna mwingine,” alisema Kileo.
 
Zitto kutwa nzima ya jana hakuweza kupatikana kwa njia ya simu kufafanua mashitaka aliyofungua polisi. Simu zake zote za kiganjani zilikuwa zimezimwa.
 
-Tanzania daima.

Read more ...

MAAJABU…NYOKA WAMFANYIA MTU MASAJI KWA GHARAMA YA $47...! CHEKI PICHA ZA TUKIO HAPA


UNAPENDA kufanyiwa masaji na nyoka? Unaweza kukaza roho na usiogope kung’atwa? Kama ndio basi nenda nchini Indonesia utaipata kwa raha zako.


Masaji hiyo inapatikana Bali Heritage Reflexology and Spa huko Jakarta, Indonesia ambako wanaweza kukuondolea uchovu wako wa siku nzima kwa massage ya nguvu inayofanywa na nyoka mkubwa.

Masaji hiyo inafanyika kwa nyoka huyo kuwekwa juu ya mwili wa mteja na mengine huachiwa yeye nyoka afanya yake. Ili kupata huduma hii mteja hutakiwa kulipa dola 47 ambazo ni zaidi ya shilingi 76,000 za Tanzania.
Read more ...

Maiti hufukuliwa makaburini ili kubadilishwa nguo huko Indonesia


Pichani ni baadhi ya wafu waliofukuliwa kaburini na kuvishwa nguo Indonesia.



KILA mwaka huko Tana Toraja, Indonesia, wafu (au maiti) hufukuliwa kutoka makaburini ili kubadilishwa nguo. Watu wa eneo hilo wa kabila la Toraja wana mila za ajabu kuhusu vifo na
maisha yanayofuata baada ya mtu kufa.

Wao mtu akifa hutakiwa kuzikwa katika eneo alilozaliwa na si lazima azikwe katika eneo alilofia.
Idadi kubwa ya watu wa eneo hilo ni Wakristo, wanaofuata ni  Waislam  na wengine ni Wapagani ambao wanajulikana kwa imani  au madhehebu ya Aluk To Dolo yaani “Njia ya Mababu”.

Torajan huishi katika maeneo ya milimani na hawataki kujulikana sana katika jamii, japokuwa wana mila na desturi zao zilizoenea katika jimbo la Sulawesi.
Read more ...

KIBURI YAPESA::PREZZO AONYESHA BUNDUKI YAKE YA "AK 47" IKIWA NI YA DHAHABU TUPU.!!

 Rapcellency, da prezident na mfalme wa bling Prezzo wa 254 ameamua kukata vilimilimi vya haters wake kwa kuamua kumuweka hadharani mlinzi wake, bunduki ya AK 47, na kikubwa zaidi ni Gold Plated .

Prezzo amekuwa akizungumza na haters wake kwa vitendo, kwa kupost Instagram picha mbalimbali zinazoonesha kuwa hana ‘njaa’ kama walivyowahi kusema baadhi ya ‘maadui’ zake wakiwemo Huddah pamoja na dada mwingine aitwaye Ashley Toto waliowahi kusema amepigika


.
Katika picha ya bunduki Prezzo aliandika “Nobody lied…….. iam a star & got a chopper in the car #TrulyUnruly #Rapcellency”
Katika picha nyingine shemeji yetu Prezzo ameonesha saa yake ya Rolex pamoja na pete vyote vikiwa ni Gold.




“I know u want the finer things in life & I can get em 4 u, all u have to do is decide how bad u want em’ #Rolex KissThePinkyRing #Rapcellency #TrulyUnruly” aliandika Prezzo katika picha hii
Read more ...

APIGIWA SIMU NA SMS ZAIDI YA MARA 40 KUTOKA KWA SHETANI


Mama mmoja toka Colorado nchini Marekani alipokea simu ya ajabu usiku mmoja wa manane kutoka kwenye namba 1-666-666-666 na ndani ya masaa machache alipokea meseji nyingi sana kutoka namba tofuti tofauti na zote zikiwa zimeandika ‘Satan’ kwa maana ya 'Shetani'.


Mwanamke huyo, Jenn Vest kipindi kipindi anatumiwa meseji hizo alikuwa anasinzia wakati akiwa bado anaendelea kumnyonyesha mtoto wake na ndipo aliposikia simu inaita ikipigwa kutoka namba 1-666-666-666.
Read more ...

LIJUE GARI JIPYA KABISA LINALOJIENDESHA LENYEWE:

Taarifa ikufikie kutoka Samukawa, Kanagawa Japan ambako stori kwenye headlines ni kampuni ya Nissan kupata furaha kubwa baada ya kufanikiwa kwa jaribio la gariwalilolitengeneza ambalo linajiendesha lenyewe. Unaambiwa limetembea umbali wa kilometa 2.3 likijaribiwa kwenye mikikimikiki ya aina mbalimbali barabarani kama vile kuovertake, kufata alama za barabarani, taa za kuongozea magari na hata sehemu za watu kuvuka barabara.




Nissan wamesema wanalengo la kuanza kuliuza hili gari miaka saba kutoka sasa, hiyo itakua mwaka 2020 ambapo gari hili lina kamera maalum pamoja na sensors zinazofanikisha kulipa taarifa ya tukio husika kwa wakati huo ndio maana linaweza kufanya kama inavyotakiwa mfano kushika breki, kukanyaga mafuta na vitu vingine.
Kingine cha kushangaza, kwa mfano kwenye miji mikubwa ambayo parking ni tatizo unaweza kuliacha likajiendesha lenyewe kwenda kutafuta parking wakati wewe unawahi mahali alafu ukimaliza shughuli zako unalikuta linakusubiri likiwa limepaki vizuri kabisa.
Baada ya kutazama hizo picha hapo juu, unaweza kutazama hii video kujiridhisha kikamilifu aisee japo hii video sio ya majaribio yaliyofanyika saa kadhaa zilizopita..
Read more ...

DIAMOND BAADA YA KUTANGAZA AJIRA SASA ATANGAZA DEMU ANAYEMPENDA JE WAMJUA

UKIFIKA katika mtaa anaoishi mwanamuziki Diamond maeneo ya Sinza Mori jijini Dar es Salaam utaanza kuhisi kuwa kuna staa anayeishi maeneo hayo, macho ya wengi huanza kumtazama mtu anayeelekea katika geti la nyumba anayoishi msanii huyo. (HM)
Muda wote geti hilo limefungwa. Ili uweze kuingia ndani itakulazimu ubonyeze kengele itakayoashiria kuwa kuna mgeni nje anahitaji kuingia ndani. Hata hivyo hauwezi kupenya kirahisi ndani hadi uulizwe shida yako na kama hauna miadi na mtu yeyote anayeishi ndani ya nyumba hiyo haitakuwa rahisi kuingia.
Mwanaspoti lilitinga katika nyumba ya msanii huyo
na kushuhudia ukimya wa hali ya juu ilhali kuna watu ndani. Baada ya kufunguliwa geti tuliingia ndani na kupokewa na Diamond aliyekuwa ameketi katika sebule iliyonakshiwa na mapambo makini ukutani huku ikiwa na samani chache lakini za gharama kubwa.
Tulitumia saa mbili mfululizo katika mahojiano na Diamond ambaye alifunguka kwa kila swali aliloulizwa na kujibu kwa ufasaha na ufafanuzi mpana.
Mwanaspoti: Utendaji kazi wako ukoje katika muziki?
Diamond: Nina mipango makini katika kazi zangu. Mambo yote lazima yapitie kwa meneja wangu ndipo yanifikie mimi, mara nyingi mtu hawezi kuzungumza na mimi moja kwa moja lazima apite huko na hiyo ndiyo staili ya Diamond. Nimejipanga kuhakikisha nafanya kazi gani, kwa wakati gani na sikurupuki tu, japo katika utengenezaji wa nyimbo zangu naweza nikapata wazo basi hapo hapo nikatengeneza mistari.
Mwanaspoti: Utendaji kazi wako ukoje kuanzia asubuhi hadi jioni?
Diamond: Saa tano asubuhi, nikishaamka kitu cha kwanza ni kwenda 'gym', mara nyingi ni hapa nyumbani kama unavyoona hapo nje kuna sehemu ya mazoezi na sehemu
nyingine zilizopo ndani, mara nyingi hutumia muda wa saa moja. Ifikapo saa sita na nusu huwa naanza kufanya kazi zangu lakini itategemea na ratiba zangu za siku ambazo ndio mwongozo wangu wa kuimaliza siku. Baada ya hapo napumzika kwa muda fulani na baadaye jioni huendelea na kazi na mara nyingi kazi zangu huwa nazimaliza usiku wa manane.
Mwanaspoti: Unalala saa ngapi? Na unalala kwa muda gani?
Diamond: Muda wangu wa kulala mara nyingi ni saa kumi na moja alfajiri na kama sikuwa na kazi nyingi studio basi nitalala saa nane usiku. Muda wangu wa kulala ni saa sita mpaka nane kwa siku. Ila hata kama nikilala mapema kuamka ni saa tano asubuhi ila itategemea na nini ninakifanya siku inayofuata na kama nina kazi maalumu na ya mapema itanilazimu niamke mapema ili kuzikamilisha.
Mwanaspoti: Shughuli gani zinazokuchelewesha mara kwa mara kulala?
Diamond: Ni kurekodi na wakati mwingine shoo. Kwa wiki ninafanya shoo nyingi, kama ni tatu basi siku zote tatu nitalala alfajiri. Siku nyingine zinazosalia ninalala usiku wa manane kwa kuwa huwa nakuwa studio na sehemu nyingine ambazo hunilazimu kufanya kazi kwa kipindi kirefu usiku.
Mwanaspoti: Kati ya usiku na mchana ni muda upi unaopenda kurekodi?
Diamond: Kazi zangu narekodi usiku na ndiyo muda ninaopendelea zaidi. Mara nyingi napenda kurekodi saa 7 usiku ili niwe na muda na saa nyingine ni kuepuka lawama kurekodi mchana, kwasababu vijana wengi chipukizi wataona napendelewa. Unajua ninapoingia studio napenda kufanya kazi kwa muda mrefu, hata hivyo iliyo bora sifanyi bora liende na siwezi kufanya kazi na prodyuza anayenipeleka tu, ni lazima na mimi nipime kama kazi niliyoifanya inakwenda vile ninavyotaka au kama yeye anavyotaka ilimradi tufanye kazi nzuri na iliyo bora.
Mwanaspoti: Unatumia muda gani kurekodi singo moja na kwa upande wa video ni siku ngapi?
Diamond: Inategemea, inaweza kuwa siku mbili au miezi sita lakini nyimbo nyingi zinatumia muda mwingi kwasababu wakati mwingine naanza halafu napata shoo hivyo inanibidi nipange muda mwingine wa kurekodi. Kuna nyimbo zangu ambazo nilizifanya kwa muda mrefu sana hizo huwa sizisahau ikiwemo Ukimwona, Mbagala, Nataka Kulewa na nyinginezo. Nakumbuka katika kazi nilizofanya kwa muda mfupi ni My Number One nilioufanya kwa prodyuza Sheddy Clever kwa kipindi kifupi sana pamoja na Mapenzi Basi sambamba na Binadamu hizi ni baadhi ya kazi ambazo hazikunipasua sana kichwa kuzikamilisha.
Mwanaspoti: Una prodyuza wako maalumu au studio yako mwenyewe?
Diamond: Sina prodyuza maalumu kila kazi nitakayotaka kuifanya ninatafuta prodyuza yule ninayemtaka hata kama sijawahi kufanya naye kazi. Ninafanya hivi nikiwa na malengo maalumu kwa kujiweka vizuri mimi kama msanii na hata kuwapa nafasi maprodyuza mbalimbali kutia mkono kwenye kazi ya mikono yangu. Ninaogopa kuwa na prodyuza maalumu kwa kuwa najua atanisumbua ikiwa atajua kwamba namtegemea yeye pekee katika kazi zangu. Studio sina kwa sasa ila nina mikakati ya kuwa na studio kwani nimeshanunua baadhi ya vifaa.
Mwanaspoti: Unadhani ndiyo sababu iliyokufanya ukagombana na Bob Junior au Manecky?
Diamond: Hapana haya mambo yalishapita lakini nilijifunza mengi ndiyo maana niliamua kuja na staili hii. Naogopa kubaki kuwa msanii ninayetegemea prodyuza fulani, bila yeye siwezi kufanya muziki, lakini mimi ni Diamond ninaweza kufanya muziki na prodyuza yeyote naye akaonyesha ufundi wake kupitia kazi yangu.
Mwanaspoti: Shoo gani kubwa kuliko zote uliyowahi kufanya ambayo haijawahi kujirudia?
Diamond: Diamond Forever. Hii ilikuwa kubwa sana ambayo sitakaa nikaisahau, ilihudhuriwa na watu wakubwa na maarufu hapa nchini hata hivyo ilikuwa ya kipekee ambayo haijafanana na yoyote ile. Ya pili ni ile ya Dar Live ambayo nilifanya baada ya kushuka katika helikopta ile pia ilikuwa kubwa. Lakini kwa nje ya nchi ni Mombasa na Comoro huko nilifanya shoo kubwa sana ambazo siwezi kuzisahau.
Mwanaspoti: Ni shoo ipi iliyowahi kukuingizia pesa kubwa kuliko zote?
Diamond: Shoo ile ya Mlimani City ya Diamond Forever, ile iliniingizia pesa kubwa sana na tangu pale ndipo nilipoanza kufurahia matunda ya kazi yangu. Nilifanya shoo pia Burundi, Mombasa na Congo shoo hizi ziliniingizia kiasi kikubwa sana cha pesa siwezi kutaja ni shilingi ngapi lakini ni pesa nyingi ambazo sitakaa nizisahau.
Mwanaspoti: Shoo ipi ilikuwa ya bei chee ambayo huwezi kuisahau
Diamond: Kwa kweli siwezi kusahau nilipofanya shoo yangu ya kwanza kubwa mwaka 2009 kwenye Fiesta iliyofanyika Dar es Salaam, ilikuwa ndiyo shoo yangu ya kwanza na kubwa wakati huo nilikuwa natamba na wimbo Kamwambie, ilinichukua muda mrefu sana kujiandaa mimi pamoja na madansa wangu wanne tulilipwa Sh 50,000 lakini sikukata tamaa kwani ilikuwa ndiyo mwanzo wangu wa kujuana na watu wengi na wadau wakubwa wa muziki hapa nchini ambao nilikutana nao kwenye ile shoo.
Mwanaspoti: Kwa hivi sasa ni shoo gani ambayo unaweza kusema kwamba utafanya kwa bei ya chini na ni shilingi ngapi?
Diamond: Shoo ninayoweza kufanya kwa bei ya chini kabisa ni Sh 10 milioni za Kitanzania na hii labda nione anayeniomba nifanye shoo hiyo hayuko vizuri na pengine ni rafiki yangu na hawezi kuninyonya, si hivyo tu itategemea pia ni kampuni gani na ni watu wa aina gani ambao watanitaka nifanye nao kazi.
Mwanaspoti: Kwa kawaida Diamond ni msanii wa gharama gani kwa shoo moja ndani na nje ya nchi?
Diamond: Kwa kawaida shoo moja ninafanya kuanzia Sh15 milioni mpaka Sh20 milioni kulingana na muda nitakaofanya shoo. Pia zile za nje ninafanya kwa gharama ya Dola 20,000 mpaka 30,000 yaani ni Sh32 milioni mpaka 48 milioni hivi kwa fedha za Tanzania na nikiwa huko nahakikisha ninafanya kazi vile inavyotakiwa. Lakini hali ni tofauti inavyokuja shoo ile ya uwanjani yaani hapa nazungumzia shoo kubwa zinazofanyika nje ya ukumbi, hizi natoza Dola 20,000 ambayo ni sawa na Sh32 milioni 32 kwa fedha ya Kitanzania.
Mwanaspoti: Kuhusu madansa wako unawachukuliaje?
Diamond: Ni kama kaka zangu na ninawapenda sana kwani tumetoka nao mbali na wanajua kuwa tunafanya kazi pamoja kutengeneza maisha hivyo ni kama ndugu zangu na tunasaidiana kwenye kila jambo ukizingatia kuwa kile tunachokipata tunagawana. Kwa kweli najitahidi sana kuwaambia hasa kuhusiana na masuala ya kimaisha, nahusika katika maisha yao ya kila siku na nijuavyo mimi nikikosea tu mmoja akapotea kundi langu litakuwa limeharibikiwa maana kila mtu namtegemea kwa upande wake. Kwa sasa wamejenga nyumba zao na wanaendelea vizuri kimaisha hilo ndilo sharti langu lazima wafanye mambo ya maendeleo kwa kile tunachokipata.
Mwanaspoti: Umesafiri nao nchi ngapi, na kwanini unapenda kuambatana nao?
Diamond: Nimesafiri nao sehemu mbalimbali kama Burundi, Comorro na sehemu nyinginezo ambako nimekwenda kufanya shoo, sina tabia ya kusafiri peke yangu hata nikienda Ulaya na hata Marekani lazima niwe nao. Ninapenda kuwa nao kwani ni sehemu ya muziki wangu na imefika wakati nimekuwa nataka mapromota kuhakikisha wanatulipia mimi na madansa wangu kwa ajili ya shoo hasa tutakapojua kuwa shoo fulani itaingiza watu wengi au udhamini mkubwa.
Mwanaspoti: Kuna safari ambayo umewahi kusafiri peke yako?
Diamond: Ziko nyingi, nilienda mwenyewe kutokana na ukubwa wa shoo, lakini ni miaka kadhaa nyuma, baadaye nilijiwekea mikakati kwamba siwezi kusafiri mwenyewe wakati shoo nahitaji kufanya na madansa wangu, awali mapromota walikuwa wagumu kunielewa na wapo waliokataa. Niliachana nao na kuwataka wakishajipanga na kuhakikisha kwamba wanaweza kunichukua mimi na madansa wangu watafanya hivyo.
Mwanaspoti: Umewahi kuwatema madansa?
Diamond: Sijawahi kubadilisha madansa kwa sababu wanajua kazi yao. Ingawa nilikuwa na madansa sita nilipokuwa naanza muziki lakini niliachana na wawili kutokana na utendaji wao wa kazi. Wawili hawa hawakuwa wabunifu kila siku walikuwa na staili ileile, niliamua kuchagua vichwa ambavyo vikikaa na mimi mwishowe tunatoka na kitu makini na chenye kueleweka. Kulikuwa na tatizo pia la kukosea stepu wakati wa shoo hili lilikuwa likinishushia sana hadhi yangu jukwaani, hapo ndipo nilipoamua kuwaondoa.
Mwanaspoti: Kwa upande wa malipo unawalipaje?
Diamond: Ninawalipa vizuri lakini siwezi kutaja kiwango ila ingekuwa kwangu ningetaja, hiyo ni haki yao wao wenyewe kutamka ila mimi siwezi kutaja. Malipo ninayowalipa yapo machoni mwa watu wanaowazunguka, dansa kujenga nyumba kumiliki baadhi ya biashara si jambo dogo, hivyo ninawalipa vizuri. Na hata gharama za kusafiri ndani na nje ya nchi vyote ni juu yangu, malipo tunayoyapata tunagawana.
Mwanaspoti: Unakumbana na changamoto zipi katika kazi yako?
Diamond: Nakumbana na mengi, kwanza unapokuwa msanii unayeongoza lazima upate vikwazo vingi. Nakumbana na watu wengi wanaonichukia na kunitusi bila sababu za msingi, hata hivyo nasingiziwa vitu vingi ambavyo havipo nadhani hii ni changamoto iliyotokana na kufanya vizuri katika muziki.
Wapo ambao wanamwona Diamond anafanya vizuri kwenye muziki badala ya kukaa na kuangalia nimepita wapi na wapi anaanza kutoa lawama kwamba ameibiwa na mengine ambayo kimsingi hayana maana.
Mwanaspoti: Siku za hivi karibuni kuna maprodyuza na wasanii wasiofahamika ambao walijaribu kutengeneza kazi yako ya My Number One na kukutusi kupitia wimbo huo na wapo waliotunga mashairi mengine yaliyozungumzia maisha yako kabla hujawa staa, ulijisikiaje? Na unachukua hatua gani?
Diamond: Awali niliumia sana nilipoibiwa mashairi ya wimbo wangu wa Mbagala, iliniuma sana kwa muda wa wiki nzima uchungu nilioupata siwezi kuuelezea. Lakini baadaye nilikomaa, huwezi amini niliposikia zile nyimbo nilicheka sana kisha nikawadharau sana watu waliofanya hivyo maana nipo kwenye hii tasnia siwezi kuchukia watu wasiojua walitendalo kwani na wao wapo katika kujitafutia riziki. Lakini hata hivyo sheria ya muziki bado haijawa makini hapa nchini
nitachukua hatua gani mwisho wa siku nitaacha kufanya mambo yangu ya msingi na kushughulikia wezi wa kazi zangu ambao hata hivyo hawatabanwa kwa lile walilolifanya.
Mwanaspoti: Msanii yupi hapa Tanzania anakutisha kama hayupo vipi huko nje ya nchi?
Diamond: Kwa hapa Tanzania sijaona mwanamuziki anayenitisha, ila siwezi kujua mashabiki wao ndio majaji, nafikiri kila mtu anaweza kuwa na mtazamo wake. Kati ya wanamuziki ninaowahusudu mimi kwa nje ya nchi hasa Afrika ni P Square pekee, hawa wapo katika nafasi kubwa sana kwenye ubongo wangu na nafikiria ni lini ninaweza kuwafikia, hiyo ndiyo ndoto yangu daima.
Mwanaspoti: Unapokuwa juu ya jukwaa unakumbana na vishawishi vipi ukiwa kama msanii mkubwa?
Diamond: Ninapata vishawishi vingi sana ninapokuwa jukwaani. Kwa kweli ninashawishiwa na wakinadada, mfano kuna mwanamke mmoja ambaye alikuwa mmoja wa mapromota wa shoo nchini Uingereza alitaka kunibusu mdomoni kwa lazima, kitendo kile kilinifedhehesha sana na nilishindwa nifanyeje kwani nipo ugenini na jukwaani ilikuwa ngumu sana kwangu. Wakati mwingine wanawake wanapanda jukwaani ili wacheze na wewe mwisho wa siku wanaingiza mikono kwenye suruali yaani sipendezwi kabisa na michezo ya namna hii.
Mwanaspoti: Umewahi kuibiwa ukiwa jukwaani?
Diamond: Nimeshaibiwa sana hasa katika hizi shoo ndogo ndogo mara nyingi watu wanapanda jukwaani na kuondoka na kitu chako. Nakumbuka nimeshawahi kuibiwa saa, pete ya dhahabu na kuna mmoja alitoa kali ya mwaka yaani yeye alinivua nguo kwa lazima.
Mwanaspoti: Inakuwaje nje ya muziki, unakumbana na changamoto zipi?
Diamond: Kitu ambacho ni changamoto kubwa sana kwangu ni simu yangu ya mkononi. Kila baada ya miezi sita au mitatu nalazimika kubadili namba yangu ya simu, nasumbuliwa sana na watu ambao hata hivyo hawana la msingi la kuniambia. Ni kweli kwamba mawasiliano ni kitu cha msingi na 
ninawapenda mashabiki wangu lakini namba yangu inasambaa kwa kasi ya ajabu kiasi kwamba nashindwa kupokea simu za maana kwa kudhani kwamba na hao nao ni wasumbufu.
Mwanaspoti: Ina maana milio yote ya simu hapo ni watu wanakupigia?
Diamond: Yap, unavyoona inalia kila dakika watu wanapiga hapa. Muda mwingi hii simu ninaweka 'silent' yaani haitoi mlio wowote kwani inaita kila dakika.
Mwanaspoti: Tuzungumzie uhusiano wako. Mpenzi wako wa kwanza unamkumbuka? na je uliwahi kumpa shilingi ngapi?
Diamond: Mpenzi wangu wa kwanza kabisa enzi hizo ninajifunza mambo haya sikumbuki vyema jina ila alikuwa anaishi Tandale na mimi pia nilikuwa naishi huko na mama yangu. Sikumbuki kama nimewahi kumhonga maana enzi hizo mimi nilikuwa napewa tu na mama yangu pesa, sikuwa na hela yoyote ya kumpa na ilikuwa ni kwa kipindi kifupi kama miezi minne hivi, hata hivyo tulikuwa tunaibana tu kwa siri nilikuwa mdogo.
Mwanaspoti: Kwanini mliachana?
Diamond: Kwanza nilikuwa sijajua mapenzi ni nini. Hata hivyo haikuwa rasmi na wala nilikuwa sijawa na akili ya kupenda sana na nilikuwa na fikra kwamba ni mchezo tu hivyo tuliachana mapema kwani hata yeye akili yake ilikuwa haijakomaa.
Mwanaspoti: Mpenzi wako uliyekuwa naye kabla ya kuwa staa nasikia uliachana naye baada ya kutoka kimuziki kwa nini?
Diamond: Nilimpenda sana lakini aliniacha kabla ya kutoka. Mpenzi wangu wa kwanza alikuwa anaitwa Sarah Sadick, sijawahi kumuhonga na ndiye mwanamke niliyewahi kumpenda sana. Wakati huo Naseeb Abdul kabla sijawa Diamond nilikuwa nahaha kuhangaika ni vipi nitatoka kimuziki. Msichana huyu ndiye aliyenipa hasira za kufanya muziki kwa bidii zote baada ya kunitema na kuanza kuhangaika na wengine na aliniita majina mengi yasiyo mazuri, kisa sina fedha. Si kwamba nilimuacha bali yeye ndiye aliyeniacha kama zali baada ya wiki kadhaa nikatoka na wimbo Kamwambie, taratibu nikaanza kuwa staa naye akaanza kurudi ila nilishamuondoa moyoni mwangu.

Mwanaspoti: Kwa nini mliachana? Unadhani hakukufaa tena kwa kuwa ulishakuwa staa?
Diamond: Alinisumbua sana kutokana na ugumu wa maisha niliokua nao kwa kipindi cha nyuma hadi kufikia 2009. Nilimpenda sana huwezi amini nilikuwa silali usingizi kwa ajili yake. Nahisi ilitokana na mimi kukosa kazi ndiyo maana ilifikia hatua alinipotezea. Lakini baada ya kupata na kujulikana alinifuata lakini sikutaka tena hata baada ya kuniomba msamaha.
Mwanaspoti: Umewahi kuwa na wanawake wangapi tangu uwe staa?
Diamond: Sikumbuki kwa kweli wapo wengi mno, si unajua tena wapo walionitaka na kunilazimisha nifanye hivyo, lakini idadi kamili siwezi kukumbuka na kila siku nasumbuliwa na hawa wanawake.
Mwanaspoti: Ni wapenzi wangapi ambao umekuwa nao kipindi kirefu na kuwapenda kama wapenzi wako?
Diamond: Nimewahi kuwa na wapenzi wanne katika kipindi chote cha ustaa wangu na sikupenda kubadili ovyo ila wengi wao hawakuweza kutimiza haja ya moyo wangu.
Mwanaspoti: Unaweza kuwataja majina?
Diamond: Ndiyo ila wawili wanafahamika zaidi. Wa kwanza kabisa alikuwa anaitwa Sarah na wa pili alikuwa anaitwa Hawa yule msichana niliyeimba naye katika wimbo 'Nitarejea', huyu alizidiwa ujanja na Wema Sepetu ambaye naye alikuja kuondoka kwangu na baadaye nikawa na Penieli Mungilwa.
Mwanaspoti: Mwanamke yupi unahisi ulimpenda kuliko wote?
Diamond: Mwanamke wangu wa kwanza Sarah Sadick huyu aliniingia sana moyoni sijajua ni kwanini. Lakini nahisi huenda kwa kuwa awali alinipenda kweli kwa kuwa wakati huo sikuwa na kitu. Hata hivyo nahisi ilitokana na mimi kutokuwa bize na wakati huo sikufikiria lolote zaidi ya yeye ilitokana na kutokuwa na kazi ya kufanya. Siku hizi sina mapenzi ya kivilee, nawaza zaidi pesa na ninaihangaikia na zaidi ni muziki wangu, hili ndilo la kwanza kabisa linalonifanya niwe bize mapenzi baadaye.
Mwanaspoti: Umeshawahi kutongozwa na wanawake?
Diamond: Ndiyo, wengi sana tena kuna mmoja kati ya wanawake niliowahi kuwa nao alinitongoza yeye mwenyewe ndipo nikawa naye na nilikaa naye katika uhusiano kwa kipindi kirefu tu. Wanaweza kumfikiria mwanamke fulani lakini huwezi amini ukweli ninao mimi mwenyewe na katu hawawezi hata kumhisi. Ninatongozwa sana kwenye mitandao ya kijamii, facebook, whatsapp, Instagram na kwingineko na wapo wasichana ambao wanatafuta namba zangu za simu na kuanza kunisumbua.
Mwanaspoti: Unapata usumbufu wowote toka kwa wanawake?
Diamond: Ndiyo, wengi sana tena kuna mmoja kati ya wanawake niliowahi kuwa nao alinitongoza yeye mwenyewe ndipo nikawa naye na nilikaa naye katika uhusiano kwa kipindi kirefu tu. Wanaweza kumfikiria mwanamke fulani lakini huwezi amini ukweli ninao mimi mwenyewe na katu hawawezi hata kumhisi. Ninatongozwa sana kwenye mitandao ya kijamii, facebook, whatsapp, Instagram na kwingineko na wapo wasichana ambao wanatafuta namba zangu za simu na kuanza kunisumbua.
Mwanaspoti: Ni mwanamke wa aina gani unataka awe mkeo?
Diamond: Kwanza ninahitaji aijue kazi yangu na ajue kwamba mimi ni mtu maarufu hivyo akubaliane na changamoto mbalimbali atakazokumbana nazo kwa kipindi atakachokuwa ndani ya ndoa, siyo siku mbili anafungasha virago. Pia ajue kwamba nitamsikiliza mama yangu kwanza kabla ya yeye hilo naliweka wazi, yeye ana nafasi yake katika maisha yangu lakini mama yangu nimempa kipaumbele, tatu awe tayari kuishi na mama yangu. Nne awe na akili na mwenye utambuzi na atakayeniongoza katika kazi zangu, sihitaji.

Read more ...

MAPENZI NOMA SANA..!! KIJANA (32) ANASWA AKIWA NA BIBI (80) CHUMBANI WAKIPONDA RAHA..!!


KUNA mengi ya kushangaza duniani lakini hili la kijana Hamad Issa (32) kunaswa faragha na bibi kizee Adela Mkalau (80) linaongeza rekodi ya mambo yanayoshangaza, Risasi Mchanganyiko lina kila kitu. Tukio hilo la kustaajabisha limetokea mwishoni mwa wiki iliyopita, nyumbani kwa bibi huyo, Yombo –Buza, jijini Dar es Salaam ambapo wajukuu wa bibi huyo ndiyo waliomnasa. Kwa mujibu wa chanzo chetu, wajukuu wa bibi huyo walifedheheshwa na kitendo hicho hivyo kuwawekea mtego na kuwanasa kisha kumfikisha Hamad katika Kituo cha Polisi Chang’ombe kwa tuhuma za ubakaji.
Katika kutafuta uhakika wa madai ya wajukuu hao, polisi wa Chang’ombe waliagiza bibi yao aitwe ili athibitishe madai hayo wakati upelelezi mwingine ukiendelea.
Sosi wetu alisema kuwa bibi aliwaacha hoi polisi baada ya kufika kituoni hapo na kukataa maelezo ya wajukuu zake, huku akisisitiza hakubakwa bali walikubaliana na Hamad. Baada ya bibi huyo kuondoa utata, polisi walikubali kumuachia Hamad kisha wajukuu wakafunguliwa kesi ya kushambulia na kudhuru mwili iliyoandikishwa kituoni hapo kwa jalada namba CHA/RB/10629/2013.
Mwandishi alifunga safari hadi nyumbani kwa bibi huyo na kuzungumza naye kuhusu tukio hilo ambapo alisema: “Sijabakwa na nimekasirishwa sana kwa kitendo cha kumpiga kijana wangu. Wawe na heshima kwa babu yao. Sisi tunapendana, kwa nini wanatuingilia?”
Alisema: “Siku hiyo Hamad wangu alikuja nyumbani kwangu tangu mapema. Nikaandaa chakula cha jioni, tukala pamoja kisha tukalala. “Tukiwa usingizini, nikasikia mlango unagongwa. Kwenda kufungua, wajukuu zangu wakaingia na kuanza kumpiga Hamad na fimbo na magongo, wakisema eti amenibaka. Hamad atanibakaje? Kwani mimi ni mtoto mdogo?
“Isitoshe wanamfahamu vizuri sana Hamad. Nipo naye  mwaka mmoja na nusu sasa, leo inakuwaje wanajifanya hawamjui? Siku hizi mambo yamebadilika. Mdogo anaweza kumpenda mkubwa na mkubwa akampenda mdogo. Hakuna kosa.”
Mwandishi wetu alikwenda nyumbani kwa Hamad ambapo alimkuta akiwa hoi kitandani kwa majeraha ambapo alisema: “Ni kweli bibi ni mpenzi wangu... na wale wajukuu zake wananifahamu vizuri sana. Wamenipiga sana, eti nimembaka bibi yao. Siyo kweli. Sisi ni wapenzi.” Alipoulizwa anajisikiaje kuwa kwenye uhusiano na kikongwe huyo, alijibu: “Hata mimi nashangaa sijui imekuwaje nikampenda. Nimejikuta nipo kwenye uhusiano naye na kwa kweli tunapendana sana.”
Mmoja wa wajukuu wa bibi huyo, Margaret Cheba, akizungumza na mwandishi wetu kuhusu tukio hilo alisema bibi yao amewadhalilisha sana na wanaona aibu kupita mitaani kwa kitendo cha kutembea na Hamad. “Hili jambo limetufedhehesha sana sisi wajukuu zake halafu hata kimila ni tatizo, hairuhusiwi kabisa. Mbaya zaidi, bibi yetu ni mgonjwa. Anasumbuliwa na moyo... sio wa kufanya kitendo kama kile kabisa na sisi ndiyo tunamsaidia lakini inashangaza polisi wametubadilikia kabisa,” alisema Cheba
Read more ...

FUMANIZI!!! KIGOGO AKAMWATWA AKIVUNJA AMRI YA SITA NA MWANAFUNZI BILA AIBU.......CHEKI HAPA


MZEE mmoja kigogo wa biashara ya kuuza mbao jijini Dar es Salaam, hivi karibuni alinaswa kitandani ndani ya chumba akiwa na mrembo aliyedaiwa ni mwanafunzi wa shule moja ya msingi Tegeta Wazo, Dar.Mfanyabiashara huyo aliyetajwa kwa jina moja la Kyando, anasemekana amekuwa na ukaribu na denti huyo anayeitwa Fatty kwa siku nyingi, kitu ambacho kiliwapa maswali baadhi ya majirani wa nyumbani kwa msichana huyo.

Katika harakati za kuchunguza ukaribu wa msichana huyo na mtu mzima huyo, mama mdogo wa binti aligundua kuwa wawili hao wana ukaribu usiofaa.

Ikaelezwa kuwa, mama mdogo wa mwanafunzi huyo aliponyetishiwa ishu hiyo, aliandaa mtego unaofyatuka kwa kasi kuliko ule wa panya ili kumtia mikononi mzee huyo mpenda kukaa na watoto wa wenzake.

“Mtego mkali uliandaliwa, siku ya siku, ma mdogo huyo alijifanya anakwenda mbali na nyumbani, binti akaona dakika tisini za mchezo lazima aibuke kidedea wa mahaba, alimwita mwanaume huyo na kumkaribisha chumbani, kumbe arobaini zao zilikuwa zimetimia,” kilisema chanzo.

Mashuhuda wa sakata hilo walidai kuwa mama mdogo na watu wengine waliwanasa wawili hao wakiwa juu ya kitanda kama walivyozaliwa, bila kufafanua walichokuwa wakikifanya.


Ili kushika ushahidi mkononi, mama mdogo wa binti huyo na wapambe wake walipiga picha za mnato na za video kisha wakaanza kumuuliza maswali ‘mlalamikiwa’ ambaye inaaminika ni mume wa mtu.

Haikuelezwa wazi ni maswali ya aina gani aliyokuwa akiulizwa lakini inadaiwa yalihusu historia ya kujuana kwao.

 Aidha, inadaiwa kuwa mama mdogo huyo alitaka kumtwanga ndoa ya mkeka mfanyabiashara huyo lakini chondechonde zake nyingi zilimwokoa na kuahidi kurejea siku inayofuata kwa ajili ya kukata mshiko wa fidia baada ya kuambiwa binti huyo bado anasoma na shuleni kulilipwa fedha nyingi.


Habari nyingine zinadai kuwa wawili hao walifahamiana miezi kadhaa nyuma kupitia lifti ya gari ambayo mshitakiwa alimpa mrembo huyo maeneo ya Boko, jijini Dar.

Read more ...

HIVI NDIVYO DIAMOND ALIVYOWEKA USTAA PEMBENI NA KUANZA KUCHEZA MZIKI USWAZIIII. CHEKI VIDEO HAPA



Read more ...

PICHA ZA UCHI..!VIDEO..!Serikali yatoa onyo kwa wanaume wanaowapiga picha za uchi wapenzi wao, ICHEKI HAPA


Serikali imesema haitavumilia mtu au kundi la watu wa aina yoyote ambao watabainika kuendeleza vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia na kutaka jamii kutumia madawati ya jinsia katika vituo vya polisi  kuripoti matukio yote ya aina hiyo ili yadhibitiwe kabla ya kuleta madhara makubwa ikiwemo watu kupoteza maisha.

Hayo yamesemwa na waziri wa  mambo ya ndani  Mh Dk Emanueli Nchimbi wakati wa uzinduzi wa dawati  la jinsia  pamoja na mpango kazi wa miaka mitatu unaaonyesha majukumu ya jeshi la polisi  katika kuimaraisha mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia.

Naye mkuu wa jeshi la polosi nchini IGP Saidi Mwema amesema tangu kuanza kufanyiwa majaribio mpango huo umeonyesha mafanikio makubwa na hivyo ameitaka jamii kujitokeza na kutumia dawati hilo.  


Akizungumza katika hadhara hiyo mratibu mkazi wa umoja wa mataifa Bw Aliberic Kacou amewataka viongozi kuhakikisha kuwa wanatumia nafasi zao pamoja na sheria zilizopo kuhakisha kuwa wanawadhibiti wale wote ambao kila mara wamekuwa wakifanya vitendo vya kikatili kwa makusudi. 

-ITV
Read more ...

MCHEKI MWANAMKE KIBAKA ATIWA NGUVUNI!!

http://tzfix.blogspot.com/2013/11/mcheki-mwanamke-kibaka-atiwa-nguvuni.html

Dada ambaye jina lake halikuweza kupatikana akizongwa na wananchi baada ya kusadikiwa kuiba simu katika moja ya duka eneo la posta barabara ya Samora na hatimaye kukimbia na kukamatwa na wananchi.
Read more ...

MAAJABU YA MUNGU!!... HUYU NDIYE MWANAUME MWENYE MOYO ULIO OTEA TUMBONI HUKO CHINA......MCHEKI HAPA

 Moyo tumboni

Ho Zhiliang, 24, raia wa China amezaliwa huku moyo wake ukiwa unaota maeneo ya tumboni kama unavyo ona kwenye picha. Kijana huyu ana subiri upasuaji ili kuweza kurekebisha kiungo hicho na kukirudisha mahali kinapotakiwa kuwa.


Kweli Mungu ni wa ajabu sana maana inasemekana watoto wengi wanao zaliwa na tatizo hili hufa siku chache baada ya kuzaliwa lakini imekuwa tofauti kwa huyu kijana ambaye ni kinyozi na ameamua kuishi maisha yake na hali hiyo hadi pale alipo soma kwenye gazeti moja kwamba hali hiyo inaweza rekebishwa kwa opareshi ambayo ndo anasubiria.
Read more ...

Tuesday 26 November 2013

BEST FEMALE ACTRESS IN TANZANIA

Tanzanian Film Industry has many top female actress talented in movie career, Most of  them being female, the listed are considered to be the best since 2007 in Tanzanian movie Industry known as “BONGO MOVIE

Name:    Irene Uwoya.
Best known for the movies of.. 
Question Mark, Apple,Safari,Zawadi Yangu, Innocent Case, Nyota Yangu, Last Card, 
Doa la Ndoa, Ngumi ya Maria, Chupa Nyeusi, Kiapo, Eagle Eyes, Diversion of Love, 
Fair Decision, Pretty Girl, Damu Moja, Shakira, Yolanda, Tanzanite.





Name:    Elizabeth Lulu Michael
Best known for the movies of..
Oxygen, Elizabeth Michael,House Boy, Ripple of Tears, Confusion,Ritazo, Family Disaster, Woman with Principal, Foolish Age.










Name:    Wema Sepetu
Best known for the movies of..

House Boy, Crazy Tenant, Basilisa, The Diary, Lerato, Tafrani, White Maria, Sakata,  Family Tears.







Name:    Skyner Ally
Best known for the movies of.. 
What is It, Why I Did Love, I Hate My Birthday’, Kizungumkuti’, Unpredictable, Shahaada 




Name:    Yobnesh Yussuph aka Batulli
Best known for the movies of.. 
Kazi Yangu, Waves of Sorrow, Fungate,Get Out, The Glory of Ramadhan, My Fiance,Ripple  of Tears, Machoz



Name:    Jacky Wolper
Best known for the movies of..
After Death, Impossible,My Princess,Tikisa, Mahaba Niue, Pain for Pain P.F.P,  Think Before,
Identity Card, Babylon, Before Wedding,I am Not Your Brother,Curse of Marriage, Ulimi, Mr.Nobody, Pusi na Paku, Lupepo Village, Hukumu ya Mande, Mtekaji, Chocolate,  End of Evil, The Diplomat, My Intention, Time After Time, Chaguo Langu, Siri ya  Moyo Wangu, God is Great, Saa4, Swadakta, Gaitan, The Impact,Mens Day Out, Dunia  Nyingine, Determination, Aching Heart, Shoga Yangu, Mafisadi wa Mapenzi, All About Love, Eagle Eyes, Wrong Decision, Mtegoni, Fake Love, Life 2 Life, Mtumwa,  Secretary, Last Minutes, Jozani.





Name:     Nargis Mohamed
Best known for the movies of.. 
Magic House, Yellow Banana, Woman with Principal




Name:     Irene Paul 
Best known for the movies of.. 
Love & Power, Kibajaji, Kalunde, Fikra Zangu, Penzi la Giza, Love Me or Love Me Not, 
I Hate My Birthday, The Shell, Handsome wa Kijiji




Name:    Shamsa Ford
Best known for the movies of..
Zawadi Yangu, Babylon, Get Out, Dont Try, I Think I hate My Wife, Loreen, 
Zawadi ya Birthday, Red Mzula, Mafisadi wa Mapenzi, Crazy Love, Saturday Morning




Name:    Salma Jabu aka Nisha
Best known for the movies of.. 
Tikisa, Subiri Mama, Matilda, I am Lost, Pusi na Paku, Mchana wa Kiza,
Kashfa Macho Yangu, Red Cross





Name:     Aunt Ezekiel
Best known for the movies of..
Pumba, Jungu la Urithi, Eyes on Me, Radio Presenter,Machozi Yangu, The Beauty Fools, 
Kijogoo, Siku za Maajabu, Best Losers, Alice & Janel, I Hate My Birthday, Lost Souls,
Mens Day Out, Shoga Yangu, Lonely Heart, The Mask, Green Light, Sound of Death,Black Sunday,Taste of Love, Endless Love, Same Girl, The Village Pastor, Wicked Love, 
The Cold Wind.




Name:     Shilole
Best known for the movies of.. 
Chungu ya Nafsi, Barmaid, Macho Yangu, Kisasi cha Jessica, Mafisadi wa Mapenzi, 
Talaka Yangu








Name:     Kajala Masanja
Best known for the movies of.. 
House Girl & Boy, Dhuluma, Shortcut, Basilisa, Devil Kingdom





Name:     Rose Ndauka
Best known for the movies of..

Waiting Soul, One Night, Fall in Love, Waves of Sorrow,Malaika,The Same Script, 
The Specialist, Real Promise, Swahiba,Kwa Heshima Ya Penzi, Love Me or Love Me Not,
Jessica, Because of You, Ruben and Angel, The Diary, Solemba,
Bad Girl, Cut Off, Sound of Death, Why Did I Love, Mahabuba







 Name:     Warda Walid
Best known for the movies of.. 
Triple L, Nipende Monalisa, The Lost Adam






Name:     Stella Premsigh
Best known for the movies of.. 
Sweet Liar.




Name:      Monalisa
Best known for the movies of..
Dakika ya Mwisho, Chai Moto, 38 Weeks, Cellular, Girlfriend.






Read more ...
Designed By Published.. Blogger Templates