Visitors


hit counter

Breaking News

728-banner


web counter

OnAir

Monday, 11 November 2013

BINTI ALIYEDAI KUWA ANA MIMBA YA DIAMOND PLATNUMZ AIBIKA NA KUTAKA KUJIUA.





Sasha, akiwa na macho makavu, alitamka mbele ya waandishi wetu kuwa mimba hiyo aliyopewa na Diamond, ilimgharimu kufukuzwa shule akiwa kidato cha nne mwaka jana.
Unadhani Sasha analo tena? Ameshaumbuka na baada ya simulizi yake ya kutunga kushtukiwa, hivi sasa mrembo huyo anatishia kujiua.
Mr. Juma ambaye ni baba mzazi wa Sasha, aliliambia Risasi Mchanganyiko: “Huyu mtoto ametishia kujiua, anajua makosa aliyoyafanya. Anataka kutuvuruga vichwa, ukweli ni kwamba kila alichokisema kuhusu Diamond ni uongo mtupu.
“Nahisi kuna mtu yupo nyuma yake, sasa anataka kumtumia ili kumchafua Diamond, upande mwingine akili yangu inaniambia yule mtoto anataka umaarufu, maana najua yule ni mwigizaji, sasa pengine anataka kutoka.”


UONGO WA SASHA
Risasi, lilipata taarifa kuhusu malalamiko ya Sasha ambaye alikuwa akidai kupotezewa dira ya maisha na Diamond kwa sababu alimpa mimba na kumtelekeza na mtoto mwenye umri wa miezi minne.
Baada ya kupata ‘tipu’ hiyo, mwandishi wetu alimsaka kwa udi na uvumba mpaka Septemba 4, mwaka huu (Jumatano ya wiki iliyopita) ambapo mrembo huyo alitia maguu kwenye mjengo mkubwa wa magazeti pendwa nchini Tanzania, Global Publishers Ltd.
Baada ya kuwasili makao makuu ya Global Publishers, Bamaga, Mwenge, Dar es Salaam, Sasha aliingizwa kwenye chumba maalum chenye mitambo ya kurekodi sauti na picha kisha akaanza kumwaga simulizi yake.
Alidai kuwa alikutana na Diamond, Mlimani City, mwaka jana, wakapeana namba za simu kabla ya kuanzisha uhusiano wa kimapenzi ambao uliwafikisha kwenye ‘kategori’ ya kuparamia kitandani na kutenda mchezo wa baba na mama pasipo kutumia na kinga.
“Nilipopata mimba Diamond alinishawishi nisitoe, akaniahidi atanisomesha hata kama nitafukuzwa shule. Baadaye nilifukuzwa shule, akazidi kunipa moyo kwamba atanilinda. Mimba ilipokuwa kubwa akapotea, nilipozaa hakujitokeza.
“Diamond akawa siyo yule ambaye alikuwa ananipa moyo. Alibadilika, hali hiyo ikanifanya nione mwanangu hana baba, hata cheti za kuzaliwa, sijamwandika Diamond, mtoto wangu nimempa ubini wa baba yangu, yaani ya Juma.”

NI UONGO MTAKATIFU
Ili kukamilisha habari hiyo ambayo ilitoka kwenye gazeti hili, toleo la Jumamosi iliyopita, mwandishi wetu aliwasiliana na baba mzazi wa Sasha (Mr. Juma) ambaye alipoambiwa kuhusu mwanaye kuzaa na Diamond, alishtuka kisha akasema:
“Unajua yule mtoto sikai naye, anaishi na mama yake. Mimi sijui chochote ila nashangaa, inawezekanaje apate mimba mpaka azae mimi baba yake sijui? Ngoja niongee na mama yake.”
Mr. Juma alipiga simu kuzungumza na mama yake Sasha mbele ya mwandishi wetu. Mazungumzo yalikuwa kama ifuatavyo;
MR. JUMA: Habari yako.
MAMA SASHA: Salama tu, za kwako?
MR. JUMA: Namshukuru Mungu, ebwana mbona Sasha kaongea na mwandishi wa habari anasema kapewa mimba na Diamond na amezaa?
MAMA SASHA: Wewe si unajua haya mambo ya vijana?
MR. JUMA: Mambo ya vijana kivipi? Ina maana mtoto anapata ujauzito mpaka anazaa wewe na baba yake hamjui?
MAMA SASHA: Baba nani, si wewe?
MR. JUMA: Mimi baba yake sijui, ndiyo maana nakuuliza wewe, maana nimesikia umekuwa unawasiliana na Diamond kuhusu hili.
MAMA SASHA: Nani kakwambia? Nimeshasema hayo ni mambo ya watoto, naomba umuulize mwanao vizuri, kama hauna namba yake nikutumie.
Katika mazungumzo hayo, Mama Sasha, hakumpa majibu ya moja kwa moja mzazi mwenzake, kuhusu binti huyo kupata mimba, kuzaa na Diamond kuwa mhusika.
cheki video yake kwa link hii 

No comments:

Post a Comment

Designed By Published.. Blogger Templates